Ingia / Jisajili

Furaha Mbughi

Mfahamu Furaha Mbughi, mtunzi wa nyimbo za Kanisa Katoliki. Kutoka Jimbo la Jimbo Katoliki la Mbeya Parokia ya Parokia ya Igogwe

Maelezo zaidi

Idadi ya nyimbo SMN: 134 > Zitazame

Jimbo analofanya utume: Jimbo Katoliki la Mbeya

Parokia anayofanya utume: Parokia ya Igogwe

Namba ya simu: 0758 972025 / 0786 847120

Soma Historia na maelezo yake hapa

Wasiliana na mtunzi kwa email:


Historia / Maelezo

Tumsifu Yesu Kristu.

Furaha Mbughi ni mtunzi na mpiga kinanda mchanga.

Napenda sana kumtumikia Mungu kwa njia ya uimbaji. Namshukuru Mungu kwa karama alizonijalia. Nilianza kuimba  kwaya mwaka 1996 wakati huo nikiwa darasa la 4. Kwasasa ni baba wa familia yenye mke na watoto wawili.

Nilianza kujifunza nota mwaka 2004, wakati huo nikiwa kidato cha tano. Na kwa mwaka huohuo nilianza kutunga nyimbo.Wimbo wangu wa kwanza kutunga ukiwa ni: "KINYWA CHANGU KITASIMULIA". mwaka jana 2016 nimetimiza miaka 20 ya uimbaji na pia miaka 12 ya utunzi. Nashukuru sana Mungu wangu kwa wema wake kwangu, namuomba aendelee kunijalia uzima na baraka nimtumikie daima!.

Kwaya ambazo nimewahi kuimba ni pamoja na:

  • Kwaya ya Mt.Cesilia _ Kigango cha Kafwafwa _Parokia ya Sange _Mbeya
  • Kwaya ya wanafunzi (TYCS) _ Shule ya Sekondari Mzumbe _Morogoro
  • Kwaya ya Mt.Cesilia _ Kigango cha Mzumbe _Parokia ya Mzumbe _Morogoro
  • Kwaya ya Mt.Thomas Moore_ Chuo Kikuu Mzumbe _Parokia ya Mzumbe _Morogoro
  • Kwaya ya Mt.Theresia wa Mtoto Yesu_Parokia ya watakatifu Petro na Paulo-Tukuyu_Mbeya
  • Kwaya ya Mt.Cesilia _ Kigango cha Igogwe _Parokia ya Igogwe _Mbeya
  • Kwaya ya Mt.Bikira Maria _ Kigango cha Igogwe _Parokia ya Igogwe _Mbeya