Ingia / Jisajili

Hapa We Msafiri

Mtunzi: Fr. Gregory F. Kayeta
> Tazama Nyimbo nyingine za Fr. Gregory F. Kayeta

Makundi Nyimbo: Mazishi

Umepakiwa na: Yudathadei Chitopela

Umepakuliwa mara 15,174 | Umetazamwa mara 27,258

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo


FR. G.F. KAYETA

MBEYA CATHEDRAL

1.     Hapa we msafiri simama na tazama, simama na tazama Nimekufa leo (kesho) ni zamu yako (ona) ona vema nilivyowekwa humu na nilivyo acha mali na jamaa.

2.     Nilitoka uchi tumboni mwa mama yangu (Tumboni mwa mamangu) na kurudi uchi (kati)ka tumbo la nchi (sanda) sanda moja hilo ni vazi langu, wameninyang'anya hata senti moja.

3.     Nifunike vema na hilo jembe lako (na hilo jembe lako) nilitangatanga (kati)ka ulimwengu (basi) Basi leo kiburi kimekwisha, kumbe dunia hii ni mti mkavu.

4.     Nyumba yangu leo ni shimo udongoni (ni shimo udongoni) hakuna mlango (haku)na madirisha (kita) kitanda changu na Blanketi langu, Ni udongo mzito wanielemea.

5.     Kifafanuacho watu mbele ya Mungu (watu mbele ya Mungu) si cheo kikubwa (sida)raja sisifa (mate)matendo mema saa ya kufa kwangu, yatafungua mlango wa mbinguni (au) (uwingu).

6.     Ole wangu mimi nilifanya ujinga (Nilifanya ujinga) kwa kuambatana (nawa)tu wa dunia (ona) ona leo wote wameniacha, Hasa watu wale niliowapenda.

7.     Unaponiona jiwazie mwenyewe (Jiwazie mwenyewe) kufa siku moja (kwa wo)te ni lazima (japo) Sultani japo ni mtumwa, Mungu atamwita ikiwa saa yake.

8.     Nimekufa leo nilipona salama (Nilipona salama) nilijishania (mwenye) Afya mwilini (nama) Na mara moja nikaanguka chini; Labda huamini kwamba nalimzima.

9.     Yesu msalabani kateswa vikali mno (kateswa vikali mno) kwa kutukomboa (Aka) mwaga damuye (wahu)wahurumie wote wa toharani, Mwanga wa milele uwaangazie.

10.   Kwaherini wote kwaherini wapenzi (kwaherini wapenzi) Nimekwenda kwetu (sita)rudi nyumbani (kwahe)rini Baba kwaheri Mama yangu, Mungu akipenda kwake tukutane.

                        


Maoni - Toa Maoni

Revocatus James ng'oja Nov 04, 2019
Wimbo mzuri unitafarishao safari yangu katika dunia hii....

Venalius Kafuba Dec 02, 2018
Mungu amlaze mahali pema peponi Amina. Ni mmojawapo wa nyimbo za kwenye CD tuliyotoa kwaya kuu parokia ya Mwanjerwa (Mt. Francisco wa Asis) na CD inayochezwa sana na Radio Maria hakika hizi nyimbo huwa zinanifariji sana kila nizisikiapo

David Nov 30, 2018
Ntaupataje huo wimbo? kwa kweli nimeupenda mno

Fredy joash Sep 14, 2018
Jamani mungu amlaze mali peponi amina. Naposikiliza aya manen kiukwel naumia sana.

Veronica Francis Buja Oct 20, 2017
Ni wimbo mzuri sana, wenye maneno mazito unaonitafakarisha sana. Kila nikiusikia huwa natoa machozi. Mungu ampumzishe kwa amani mtunzi.

stanslaus kamalamo Jan 04, 2017
naupenda sana,hapa we msafiri

Toa Maoni yako hapa