Ingia / Jisajili

Niseme Nini?

Mtunzi: Bernard Mukasa
> Mfahamu Zaidi Bernard Mukasa
> Tazama Nyimbo nyingine za Bernard Mukasa

Makundi Nyimbo: Shukrani

Umepakiwa na: Bernard Mukasa

Umepakuliwa mara 33,529 | Umetazamwa mara 50,015

Download Nota
Maneno ya wimbo

KIITIKIO:

Niseme nini Ee Bwana? Nitamke maneno gani kinywani? Nikushuru jinsi gani?

Nisimulie vipi mimi, mapito niliyopita kuja hapa? Nikutukuze vipi Mungu?

Niseme tu (Bwana) Mungu (wangu); asante nakushukuru. Narudia (Bwana) Mungu (wangu); Asante nakushukuru.

1. Nakumbuka nilivyojaribu; Sikujua kama utajibu; nikapapasa mkono gizani, kulipokucha ni tunda mkononi.

2. Katikati ya safari maji yote yakamwagika chini. Lakini kwa wema wako ukayazoa yakajaa upya.

3. Nilipigwa mawe, nikaaibishwa mimi, tazama leo umeniona; ukamtukuza mtumishi wako.


Maoni - Toa Maoni

Romwald M.Amos Mar 22, 2020
Hongera sana kwa utunzi wako mzr wa nyimbo,ww pia ni hazina katika Kanisa Katoliki

Alex Komba Jun 24, 2019
Hongera sana Mwalimu Bernard Mukasa! Your songs are really inspiring!!

John njuki Apr 11, 2019
Heko bwana Mukasa.Nyimbo zako hasa huu wimbo hunibariki sana.

Deogratius Oct 21, 2018
Ni Kati ya nyimbo nazozipend San... Nakuombea Sana Mukasa...

Paul Nzomo Sep 18, 2018
Huu wimbo umenibariki sana,asante Mungu kwa ajili ya mtumishi wako benard,mbariki azidi kukutumikia

Ayuto Nkweso Jul 28, 2018
nyimbo nzuri sana mim binafsi imenipendeza mno,,, hongera sana

Sir: Mathayo Msongole Sep 16, 2017
Congratulation Teacher mi nakuheshimu sana. Karibu Baraza la Maaskofu TEC ndugu japo kutupa hai. Big up

Fred Mhiche Aug 18, 2017
Bernard, you always bring me closer to God through your songs. Your songs make me meditate deeply and deeply. I am graced to live in this era of your presence. Be blessed abundantly.

Benard Kashonele Mar 22, 2017
Ni nyimbo nyingi zmenibariki na kunigsa lakini katika huu wimbo wako wa shukrani ndugu BERNARD MUKASA nakupongeza sana. kweli napata faraja na matumaini tele na wanikumbusha kurejea mapito mengi magumu na mepesi na kumwambia MNGU asante kwan yatupasa kushukuru kwa kila jambo. Mungu akubariki sana na abariki kaz ya mikono yako.

Boniface Mutula Mar 20, 2017
kazi nzuri sana mwalimu mukasa.ningependelea sana tupatane

Adam Kamanda Feb 28, 2017
Bernard. Toka nasoma na wewe Primary nimekuwa mpenzi wa nyimbo zako. Hongera sana kwa kazi hii. Naomba unitafute namimi nichangie sehemu ya usambazwaji wa nyimbo hii. Asante sana. Hongera sana.

Jasper Jan 30, 2017
Kazi nzuri sana in wimbo unaonibariki katika furaha Na misukosuko ya maisha ..... nawezaje kupakua audio yake????

Aidanus Chimazi. Jan 17, 2017
Hongera sana bernard,,,,,,,, Mungu akujalie maisha marefu kwa kazi zako nzuri na zenye kuvuta makini ya wasikilizaji

simon samora Sep 21, 2016
Hongera sana mwl mkasa napenda sana nymbo zako... Hasa huu niseme nini ee bwana... Hv umeshatoa video yake

Abel kilimtali Jul 24, 2016
Ubarikiwe sana Mukasa napenda sana kazi zako zinatoa tafakari ya kina sana pia zinanibariki sana

Abel kilimtali Jul 24, 2016
Ubarikiwe sana Mukasa napenda sana kazi zako zinatoa tafakari ya kina sana pia zinanibariki sana

Regina Stephen Jul 03, 2016
Pongeza, Koa.... Uwe mstaarabu kwakweli hata leo nimeua niuanfike kabisa siwezi kuanza chochote bila kuuimba huu wimbo. najisikia kama nipo mbinguni. kazi nzuri saaana.Mungu azidi kuimarisha kipaji chako Smina

pierre Jun 03, 2016
Pongeza, goood

william May 22, 2016
Nakupongeza sana ndugu MUKASA Mungu akubariki sana huwa na Barikiwa sana na kazi zako,

Toa Maoni yako hapa