Ingia / Jisajili

Bwana amejaa Huruma na Neema

Mtunzi: Boniventure John Oisso
> Mfahamu Zaidi Boniventure John Oisso
> Tazama Nyimbo nyingine za Boniventure John Oisso

Makundi Nyimbo: Zaburi

Umepakiwa na: BONIVENTURE OISSO

Umepakuliwa mara 674 | Umetazamwa mara 2,009

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

( Bwana amejaa Huruma na Neema ) X2

Maashairi

1.Ee nafsi yangu umhimidi Bwana.
   Naam, vyote vilivyo ndani yangu
   Vilihimidi jina lake takatifu.
   Ee nafsi yangu umhimidi Bwana,
   Wala usizisahau fadhili zake zote.

2. Akusamehe maovu yako yote,
   Akuponya magonjwa yako yote,
   Aukomboa uhai wako na kaburi,
   Akutia taji ya fadhili na rehema.

3. Bwana ndiye afanyaye mambo ya haki,
   Na hukumu kwa wote wanaoonewa.
   Alimjulisha Mussa njia zake,
   Wana wa Israel matendo yake.

4. Bwana amejaa Huruma na Neema,
   Haoni hasira upesi, ni mwingi wa fadhili.
   Maana mbingu zilivyoinuka juu ya nchi,
   Kadiri ileile rehema zake ni kuu  kwa waamchao.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa