Ingia / Jisajili

Inuka Ee Bwana - Zaburi Ya Maandamano

Mtunzi: Br. Stan Mkombo, Ofmcap
> Tazama Nyimbo nyingine za Br. Stan Mkombo, Ofmcap

Makundi Nyimbo: Ekaristi / Komunio | Kristu Mfalme | Mafundisho / Tafakari | Matawi | Zaburi

Umepakiwa na: Stanslaus Mkombo

Umepakuliwa mara 911 | Umetazamwa mara 3,307

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

INUKA EE BWANA                                                [Br. Stanslaus Mkombo, OFMCap.]

   [Zaburi ya Maandamano, Taz. Hes 10:35; Zab. 68:1-3 & Zab 24: 7-10]

// Inuka ee Bwana, adui zako watawanyike, na hao wakuchukiao wakimbie mbele zako.//x2

1. Kama moshi upeperushwavyo, ndivyo uwapeperushavyo wao; Kama nta motoni waovu hutoweka mbele zako.

2. Bali wenye haki hufurahi, huushangilia uso wa Mungu; hupiga kelele kwa furaha kumshukuru Mungu wao.

3. Inukeni enyi malango, enyi malango ya milele; Bwana na Mfalme wa Utukufu apate kuingia.

4. Nani Mfalme wa Utukufu? Bwana mwenye nguvu, hodari; Bwana mungu wa majeshi hodari hodari wa vita.


Maoni - Toa Maoni

bragon Skauti Ritte Mar 31, 2018
Umejitahidi kutunga ongeza bidii

Toa Maoni yako hapa