Ingia / Jisajili

Jiwe Walilolikataa Waashi

Mtunzi: Alfred Ogombo
> Mfahamu Zaidi Alfred Ogombo
> Tazama Nyimbo nyingine za Alfred Ogombo

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari

Umepakiwa na: Alfred Ogombo

Umepakuliwa mara 1,526 | Umetazamwa mara 6,591

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

 Jiwe walilolikataa waashi – limekuwa jiwe kuu la pembeni

Jiwe walilolikataa waashi (jiwe hilo) limekuwa jiwe kuu

la pembeni x2

1.Kwa hiyo wekeni mbali nanyi uovu wote, na udanganyifu wote

   unafiki, wivu na masingizio ya kila namna

2.Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa,

   yatamanini maziwa ya kiroho (yasiyoghoshiwa ili kwa hayo mpate)

   kuukulia wokovu ikiwa kweli – mmeonja ya kwamba

   Bwana ni mwema Mwendeeni Yeye aliye jiwe lililo hai,

   lililokataliwa na wanadamu bali – kwa Mungu ni teule na la thamani

   kwake

3.Ninyi nanyi kama mawe yaliyo hai, mmejengwa kuwa nyumba ya

   Roho, mpate kuwa ukuhani, mtakatifu mkitoa dhabihu za kiroho

   zinazokubaliwa – na Mungu kwa njia ya Yesu Kristu


Maoni - Toa Maoni

Onesmo Mlahagwa Apr 30, 2018
Mzur lakn kinanda bado ongeza juhudi

Toa Maoni yako hapa