Ingia / Jisajili

Mashujaa Wake Bwana

Mtunzi: Br. Stan Mkombo, Ofmcap
> Tazama Nyimbo nyingine za Br. Stan Mkombo, Ofmcap

Makundi Nyimbo: Watakatifu | Mafundisho / Tafakari

Umepakiwa na: Stanslaus Mkombo

Umepakuliwa mara 810 | Umetazamwa mara 2,671

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

HAWA NDIO MASHUJAA WA BWANA                                                                                                      [Br. Stan. Mkombo, OFM cap]

(I:Hawa ndio mashujaa wake Bwana) Hawa ndio mashujaa wake Bwana:

Walibatizwa ubatizo wa Bwana wao, wakapanda Kanisa kwa damu yao.

Waliukabili vema mslaba wao wakamaliza kazi na wakashinda;

[(I&II: Walikinywea kikombe chake Bwana) Hata wakawa marafiki wake Mungu. ]x2

1.     Ndugu zetu wameshinda kwa damu ya mwanakondoo, na kwa nguvu ya ukweli ule walioutangaza; hawakuyathamini maisha yao kuwa kitu sana: (I&III) Kwa ajili ya Jina la Bwana walikuwa tayari kufa x2

2.     Machoni pa watu wajinga walionekana wamekufa, na kufariki kwao kulidhaniwa kuwa ni hasara yao; Lakini wako mbele ya kiti cha enzi chake Mungu: (I&III) Nao wamtumikia Bwana mchana hata usiku x2

3.     Naye Mungu atafanya makao yake katia yao, watakuwa watu wake naye atakuwa Mungu wao; Naye atayafuta machozi katika macho yao: (I&III) Ndipo hakutakuwa na kifo maumivu wala kilio x2

4.     Watatawala pamoja naye, na kung’aa kama nyota mbinguni, kwani mungu kawajaribu na kuwaona wamestahili. Kama dhahabu katika tanuru aliwajabu: (I&III) Kisha Bwana akawakubali kwa mfano wa kafara x2


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa