Ingia / Jisajili

Mungu Ameniteua Nilihubiri

Mtunzi: Alfred Ogombo
> Mfahamu Zaidi Alfred Ogombo
> Tazama Nyimbo nyingine za Alfred Ogombo

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari

Umepakiwa na: Alfred Ogombo

Umepakuliwa mara 760 | Umetazamwa mara 2,323

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

1.Mungu ameniteua nilihubiri,

   ni wajibu wangu kulihubiri neno

   Kwa mataifa mbali mbali mataifa,

   neno na lipenye kote lipenye kote

Mafundisho ya Bwana ni ngao yangu mimi, ni wapo vitani, dhidi ya shetani

Mafundisho haya hakika ni taa yangu, kuangaza njia, ya kufuata mimi

2.Neno lake Bwana ndugu halibagui,

   kwani sote tuko sawa mbele ya Mungu

   Analotaka Bwana tunyenyekee,

   Tumakinike na tulisikize neno

3.Neno lake Bwana limejaa msamaha,

   tumaini la uzima sote twapata

   Vile yatupasa kuishi maisha yetu,

   Bibilia ndilo mwongozo kamili

4.Neno la hekima ndilo neno la Bwana,

   neno la wokovu ndilo neno la Bwana

   Neno la uponyaji ndilo neno la Bwana,

   neno la uhuru ndilo neno la Bwana

5.Akina baba wote msikie neno,

   akina mama wote msikie neno

   Nao vijana wote msikie neno,

   nanyi watoto wote msikie neno


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa