Ingia / Jisajili

Ninapokula Mwili Wa Kristo

Mtunzi: David B. Wasonga
> Mfahamu Zaidi David B. Wasonga
> Tazama Nyimbo nyingine za David B. Wasonga

Makundi Nyimbo: Ekaristi / Komunio | Juma Kuu

Umepakiwa na: David Wasonga

Umepakuliwa mara 1,681 | Umetazamwa mara 5,131

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Kiitikio:

Ninapokula mwili wa Kristo na kuinywa damu yake natangaza kifo chake na kuutukuza ufufuko wake

Mashairi:

1. Niulapo mwili wa Kristo na kuinywa damu yake, ninakaa ndani yake naye hukaa ndani yangu.

2. Mwili wa Kristo ni chakula bora, ni chakula cha roho zetu, hushibisha nafsi zetu ndiyo tulizo la roho zetu.

3.Damu ya Kristo ni kinywaji safi, ni kinywaji cha roho zetu, hushibisha nafsi zetu ndiyo tulizo la roho zetu.

4. Huu ndio mwili wangu ulio kwaajili yenu, fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu, fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.

5.Hii ndiyo damu yangu iliyomwagika kwa ajili yenu, fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu, fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa