Ingia / Jisajili

Sala Ni Nini

Mtunzi: Filbert Munywambele (Fimu)
> Tazama Nyimbo nyingine za Filbert Munywambele (Fimu)

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari

Umepakiwa na: Basil Tumaini

Umepakuliwa mara 878 | Umetazamwa mara 4,106

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

SALA NI NINI

Na. Filbert Munywambele

Kiitikio:

Sala ni nini ndugu yangu? Hebu nieleze.

Sala nimazungumzo na Mungu wetu x 2

kuinua moyo na akili kwake na kuyatafakari matendo yake kwetu. X 2

Tusali pamoja katika familia, tusali pamoja katika jumuia/

Tuombe amani katika nchi yetu, tuombe amani katika bara letu.

 

Mashairi:

1.    Sala ni mahusiano yakinifu na Mungu, inahitaji umakini, uaminifu, usikivu kati yako na Mungu wako.

2.    Sala ni kuonesha hisia zetu, kufungua moyo wetu na akili zetu kwa Mungu.

3.    Sala ni kujiweka mbele ya Mungu, mkutano wa upendo Mungu na binadamu

4.    Sala ni kumwendea aliye juu: Utatu mtakatifu, Mungu mmoja.


Maoni - Toa Maoni

Mathew Elisha Suleiman Nov 22, 2017
Nimebarikiwa kwa fafanuzi hasa ya sala.Barikiwa na Yesu .kazi yako ni njema.

Toa Maoni yako hapa