Ingia / Jisajili

Sekwensia ya Mwili na Damu ya Yesu (Ekaristi)

Mtunzi: F. K. Wambua
> Tazama Nyimbo nyingine za F. K. Wambua

Makundi Nyimbo: Ekaristi / Komunio

Umepakiwa na: Eusebius Joseph Mikongoti

Umepakuliwa mara 1,324 | Umetazamwa mara 3,891

Download Nota
Maneno ya wimbo
SEKWENZIA(SHEREHE YA MWILI NA DAMU YA BWANA WETU YESU KRISTU)

1. Ee Sayuni umtukuze, uwezavyo umwimbie mkombozi na Mwalimu, apitaye kila sifa (Kwa nyimbo na shangwe kuu, itokayo kwao watu) x2
2. Ee Mchungaji wetu mwema, Yesu utuhurumie utuchunge utulinde, ewe mlinzi wetu mwema (Utupe me_ma yako, kwenye raha ya milele) x2
3. Ni mkate wa Malaika, huwalisha wasafiri kweli mkate wa_ wana, usitupwe kwao mbwa (mifano ya_ zamani, kutolewa kwa Isaka) x2
4. Hula wema pia wabaya, kwa bahati mbali mbali kifo au U_zima, basi mkate mtakatifu (ni sumu kwa_ wabaya, dawa bora kwao wema) x2
5. Ikimegwa hii sakramenti, usisite kuamini huwa ndani ya kipande, mwili wote wake Yesu (ya kwamba ha_umegwi, ni alama ivunjwayo)x2
6. Ee Mchungaji wetu mwema, ee mwenyezi na mjuaji mwenye kutuchunga hapa, tujaliwe pia huko (tushiriki meza moja, na raia wa mbingu) x2

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa