Ingia / Jisajili

Shamba La Mizabibu

Mtunzi: Alan Mvano
> Mfahamu Zaidi Alan Mvano
> Tazama Nyimbo nyingine za Alan Mvano

Makundi Nyimbo: Zaburi

Umepakiwa na: Alan Mvano

Umepakuliwa mara 2,830 | Umetazamwa mara 5,665

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Kiitikio

Shamba la mizabibu la Bwana, Shamba la mizabibu la Bwana

ndilo nyumba ya Israeli, ndilo nyumba ya Israeli.

Mashairi

1.Ulileta mizabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda

    nao uliyaeneza matawi yake hata baharini, na vichipukizi vyake hata kunako mto

2. kwanini umezibomoa kuta zake, wakuchuma wote wapitao njiani ?

    nguruwe wa msituni wanauharibu, na hayawani wa kondeni wanautafuna

3. Ee Mungu wa majeshi tunakusihi urudi, utazame toka juu uone, uujilie mzabibu huu,

    na mche ule ulioupanda, kwa mkono wako wa kuume

4. Basi hatutakuacha kwa kurudi nyuma, utuhuishe nasi tutaliitia jina lako,

    Ee Bwana Mungu wa majeshi uturudishe, uangazishe uso wako nasi tutaokoka


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa