Ingia / Jisajili

Tumwimbie Mwokozi Wetu (Utamaduni)

Mtunzi: Reuben Maghembe
> Tazama Nyimbo nyingine za Reuben Maghembe

Makundi Nyimbo: Anthem | Mwaka Mpya | Noeli | Pasaka | Tenzi za Kiswahili

Umepakiwa na: Reuben Maghembe

Umepakuliwa mara 997 | Umetazamwa mara 3,081

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

KIITIKIO

Njoni waumini (njoni nyote), njoni waumini (njoni) sote tumwimbie Mungu wetu. Tucheze (na) ngoma za kikwetu tutangaze sifa zake *2

Tucheze tamaduni zetu njoni watu wa nchi zote tumwimbie Mwokozi wetu

Malaika wa mbinguni wanaimba kwa shangwe kuu aleluya, aleluya watu wote pigeni makofi kwa shangwe tumwimbie Mwokozi wetu*2

MASHAIRI

1. Aleluya aleluya tuimbe sote aleluya aleluya, aleluya tutazitangaza sifa zake

2. Wanyama wote wa nchi na wa maji, na waushangilie utukufu wa Mungu kwa maana yeye ndiye Muumba vyote

3.Wafugaji na wakulima wa mazao yote walisifu jina lake Bwana. Wafanyakazi matajiri na wafanya biashara walitangaze jina lake

4. Ndege wa angani wanaruka, kutangaza utukufu wa Muumba wetu na ukamilifu wa neno lake aleluya

5.Makabila yote na yamtukuze mwenye enzi kwa vinubi, kwa vinanda na kwa ngoma za asili na kengele


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa