Ingia / Jisajili

Zaburi Ya Kwanza

Mtunzi: David B. Wasonga
> Mfahamu Zaidi David B. Wasonga
> Tazama Nyimbo nyingine za David B. Wasonga

Makundi Nyimbo: Zaburi

Umepakiwa na: David Wasonga

Umepakuliwa mara 1,661 | Umetazamwa mara 10,028

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Kiitikio:

Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki, wala hakusimama katika njia ya wakosaji, wala hakuketi barazani pa wenye mizaha, bali sheria ya bwana ndiyo impendezayo, na sheria yake huitafakari mchana na usiku.

Mashairi:

1. Naye atakuwa kama mti uliopandwa kandokando ya vijito vya maji, uzaao matunda yake kwa majira yake, wala tawi halinyauki na kila alitendalo litafanikiwa.

2. Sivyo walivyo wasio haki, hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo, kwa hiyo wenye haki hawatasimama hukumuni,wala wakosaji katika kusanyiko la wenye haki.

3.Kwa kuwa Bwana anaijua njia ya wenye haki, bali njia ya wasio haki itapotea. 


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa