Ingia / Jisajili

Himery Msigwa

Mfahamu Himery Msigwa, mtunzi wa nyimbo za Kanisa Katoliki. Kutoka Jimbo la songea Parokia ya Familia takatifu - bombambili

Maelezo zaidi

Idadi ya nyimbo SMN: 324 > Zitazame

Jimbo analofanya utume: songea

Parokia anayofanya utume: Familia takatifu - bombambili

Namba ya simu: 0758149997, 0626905315

Soma Historia na maelezo yake hapa

Wasiliana na mtunzi kwa email:


Historia / Maelezo

                Naitwa Himery Andrea Msigwa mzaliwa wa kijiji cha uhekule ndani ya mkoa wa Njombe .........Nilianza utume wa uimbaji mwaka 2012 nikiwa kidato cha tano katika shule ya wavulana Njombe sekondari (sauti ya nne) hapo ndipo safari yangu ya muziki ilipoanzia  lakini nilianza kujifunza muziki rasmi mwaka 2014 nikiwa chini ya kwaya ya Mt.Kamili chuoni dodoma (UDOM) katika kitivo cha TIBA ..........katika kwaya ndipo nilipo anza kujifunza namna ya kutunga nyimbo mbalimbali. ninamshukuru Mungu kwa kuwa bado nazidi kujifunza kila iitwapo leo..........Nawashukuru wale wote ambao walikuwa na bado wamekuwa chachu ya kuendelea kujifunza kwangu.

kwaya ambazo nilishawahi kufanya utume ni;

KWAYA YA TYCS (NJOSS ...2012-2014) ,KWAYA YA MT.KAMILI....2014-2019 (UDOM-TIBA), KWAYA YA MT.VICENT WA PAULO (SONGEA), KWAYA YA MT.PAULO MTUME..2017-2018 (KIBAHA)...KWAYA YA MOYO MTAKATIFU..2018-2019 (IRINGA-KIHESA-CATHEDRAL), MT.ANNA 2019-2020 (SUMBAWANGA -CATHEDRAL).


Utume wa uimbaji ni utume bora.."Ona tunavyounganishwa watu wa rika, makabila na shughuli mbalimbali katika utume wa kumuimbia Mungu".........Tumsifu Yesu Kristo.