Ingia / Jisajili

Yudathadei Chitopela

Mfahamu Yudathadei Chitopela, mtunzi wa nyimbo za Kanisa Katoliki. Kutoka Jimbo la Arusha Parokia ya Parokia Teule ya Utatu Mtakatifu - Morombo

Maelezo zaidi

Idadi ya nyimbo SMN: 105 > Zitazame

Jimbo analofanya utume: Arusha

Parokia anayofanya utume: Parokia Teule ya Utatu Mtakatifu - Morombo

Namba ya simu: +255 754 856 397

Soma Historia na maelezo yake hapa

Wasiliana na mtunzi kwa email:


Historia / Maelezo

Kwa sasa ni Mwanakwaya wa kwaya ya Kristo Mfalme, Parokia Teule ya Utatu Mtakatifu-Morombo Arusha.

Naimba sauti ya Nne.

Muziki ni sehemu ya maisha yangu ya kila siku.

Elimu ya Muziki ni pana sana, napenda sana kujifunza kutoka kwa watunzi wengine; unapoona kunashida katika Muziki wangu naomba sana usisite kunifahamisha. nipotayari kujifunza kutoka kwa wengine kwani mimi naamini mawazo ya wenzangu yananisaidia kuboresha nyimbo ninazotunga na ujumbe tunaotakiwa kushirikishana kama Wakristo.
Mimi ninafanya shughuli zangu binafsi za IT.
Muda wangu mwingi wa ziada nautumia katika kutunga nyimbo na  kuchora nyimbo za watunzi wenzangu ili kuweza kuzisambaza kwa wengine ili ziwezekutufaha sote watoto wa taifa la Mungu.

Nimewahi kuhumu katika kwaya zifuatazo.

1.Mt.Augustino Parokia ya K/Ndege Dodoma

2.Tabora School Choir-Tabora

3.Mt.Augustino Parokia ya Chuo kikuu DSM

4.Mt.Cesilia Parokia ya Mt.Theresia wa Mtoto Yesu-Arusha Cathedral

5.Kristo Mfalme Parokia Teule ya Utatu Mtakatifu- Morombo Arusha