Mtunzi: Elia Kalindima
> Tazama Nyimbo nyingine za Elia Kalindima
Makundi Nyimbo: Shukrani
Umepakiwa na: Elia Max
Umepakuliwa mara 0 | Umetazamwa mara 0
Download Nota Download Midi
1. Mungu Wangu, Bwana kwa moyo wa furaha nikurudishie utukufu wako kwanza. Na kwa sauti yangu,niyasimulie haya,yaimarishayo imani inifanyayo nikushukuru.
Mungu Wangu nimeona (matendo) unayonitendea, ni makuu mno kuzidi akili zangu.Hata sasa unayatenda haya,licha ya udhaifu wangu, Nina kila sababu ya kukushukuru.
{Kwa kinywa nasema Asante (unanilinda,unaniponya, sasa naleta) ushuhuda wa kweli kwa moyo nasadiki.Kwa matendo na sadaka, naleta kwako Bwana.Sina cha kulipa,nimekuja nikushukuru.}x2
2. Kila asubuhi wanijaza neema,wanipa maisha,sababu ya kujituma.Wabariki juhudi zangu za kila mchana,wanilisha, na kunilinda ninapolala.
3. Nasitajisifu kwamba nasali sana,kwa unayonipa,wala na sitojigamba.Ni kwa neema hii,nami nikaitwa mwana,najivunia nina Baba upande wangu anishindia.
Kibwagizo
Furaha,Amani (Bwana) unanijalia.Chakula,Uhai (Bwana) umenipa Bwana.
Umeyafumbua upya macho yangu,kumbe yapo tele! ya kukushukuru.
Sitarudi kale kwenye kulaumu,nisije kufuru nikajisahau.
Kwa kinywa nasema Asante (unanilinda,unaniponya, sasa naleta) ushuhuda wa kweli kwa moyo nasadiki.Kwa matendo na sadaka, naleta kwako Bwana, sitakufuru, Nitashukuru.