Mtunzi: J. Kasindi
> Tazama Nyimbo nyingine za J. Kasindi
Makundi Nyimbo: Kwaresma
Umepakiwa na: Vitus Tondelo
Umepakuliwa mara 0 | Umetazamwa mara 0
Wimbo huu unaweza kutumika:
- Katikati Ijumaa Kuu
KIITIKIO
Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu
BETI
1. Nimekukimbilia wewe , Bwana, Nisiabike milele. Kwa haki yako uniponye, Mikononi mwako naiweka roho yangu, Umenikomboa, Ee Bwana, Mungu wa kweli.
2. Kwa sababu ya watesi wangu nimekuwa laumu, Naam, hasa kwa jirani zangu; Na kitu cha kutisha kwa rafiki zangu; Walioniona njiani walinikimbia.
3. Nimesahauliwa kama mfu asiyekumbukwa; Nimekuwa kama chombo kilichovunjika. Maana nimesikia masingizio ya wengi. Hofu ziko pande zote.
4. Lakini mimi nakutumaini wewe, Bwana, Nimesema, wewe ndiwe Mungu wangu. Nyakati zangu zimo mikononi mwako; Uniponye na adui zangu.