Ingia / Jisajili

Furaha Ya Jubilei

Mtunzi: Enock Charles Mangasini
> Mfahamu Zaidi Enock Charles Mangasini
> Tazama Nyimbo nyingine za Enock Charles Mangasini

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari

Umepakiwa na: Enock Mangasini

Umepakuliwa mara 534 | Umetazamwa mara 2,548

Download Nota
Maneno ya wimbo

FURAHA YA JUBILEI- ENOCK C.MANGASINI KIITIKIO: Ni Furaha na Shangwe katika parokia , ya Kristo Mfalme, Tabata. Kwa kuadhimisha, jubilei,ya miaka, ishirini na mitano x 2 . KIBWAGIZO: (Tupige) vigelegele, nderemo na vifijo, ni furaha ( ni furaha furaha), furaha ya jubilei, ni furaha, furaha ya jubilei x2. MASHAIRI: 1. Jubilei hii ni matunda ya uimisionari, na uinjilishaji, tangu mwaka moja, tisa tisa tatu, iliposimikwa rasmi, kuwa Parokia. 2. Tunamshukuru Mwenyezi Mungu, kwa kutujalia, neema na Baraka, ili tuendelee, kumjua,Kumpenda na kumtumikia, ili tufike kwake, kule mbinguni. 3. Tunawapongeza viongozi anzilishi, hayati Kadinali Rugambwa, na Paroko Albino Tesha, kwa kuanzisha na kuweka misingi bora ya parokia. 4. Tunawapongeza viongozi wa Parokia na waamini, kwa kuwezesha, kuanzishwa, kwa Parokia mpya, ya Kristo Mchungaji Mwema, Tabata Kimanga. SHAIRI LA TANO LITASOMWA KAMA SIMULIZI 5. Tunawaombea maaskofu wetu wa Jimbo Kuu la Dar es salaam (Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo,Askofu Mkuu Mwandamizi Mhashamu Yuda Thaddeus Ruwaichi na Askofu Msaidizi Mhashamu Eusebius Alfred Nzigilwa), watawa wote, Mapadre wetu wa Parokia ya Kristo Mfalme Tabata ( Paroko Padre Cornelius John Bosco Mashare na Paroko Msaidizi Padre Christian Singano), na walei wote ili kuendelea na kazi ya Bwana.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa