Ingia / Jisajili

Jiwe Walilokataa Waashi

Mtunzi: B. Simfukwe
> Tazama Nyimbo nyingine za B. Simfukwe

Makundi Nyimbo: Pasaka

Umepakiwa na: Yudathadei Chitopela

Umepakuliwa mara 12,473 | Umetazamwa mara 19,530

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Jiwe walilokataa waashi ni (jiwe imara) limekuwa jiwe kuu la pembeni (la pembeni), limekuwa jiwe kuu la pembeni x2

  1. Bwana Mungu ndiye aliyefanya jambo hili, nalo ni la ajabu sana kwetu.

  2. Hii ndiyo siku aliyofanya Bwana Mungu, basi tushangilie kwa furaha.

  3. Utuokoe sisi sote ewe Bwana Mungu, tunakusihi utupe furaha.

  4. Abarikiwe ajae kwa jina la Bwana, alete Baraka toka mbinguni.

  5. Wewe ndiwe Mungu wangu nami nakushukuru, ninakutuza Ee Mungu wangu.

  6. Mshukuruni mwenyezi Mungu kwa kuwa ni mwema, na fadhili zake ni za milele.

Maoni - Toa Maoni

samwel Jul 26, 2016
hongereni kwa kazi ya mungu

Toa Maoni yako hapa