Ingia / Jisajili

Ndoa Yenu

Mtunzi: J. Tobias

Makundi Nyimbo: Ndoa

Umepakiwa na: FRED KITUYI

Umepakuliwa mara 1,721 | Umetazamwa mara 4,034

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

NDOA YENU (J. TOBIAS)

Kiitikio:

Bwana na bibi harusi amkeni njoo – Mungu amawaunganisha.

Leo siku ya furaha tushangilieni – heko kweli kwa Bwana Mungu.

(Ndoa yenu (Ee!) ni takatifu, ndoa yenu itasitawi (Ee!),

Mtazaa (Ee!) matunda mema yenye baraka za Mungu.) x2

   1. Mtu atamwacha babaye, atamwacha na mama yake,

                Ataambatana naye mke na kuwa mwili mmoja kweli.

              2.  Mmekuwa mwili mmoja, Bwana Mungu mwenyewe ndiye,

                   Amewaunganisha pamoja, hawezi mtu kutenganisha.

              3.  Mtazaa matunda mema, nyumba yenu iwe ya sala,

                Mkawatunze watoto wenu, kwa neno lake Mwenyezi Mungu.

              4.  Sisi sote tushangilie, Mungu wetu kwa mema yote,

                  Vigelegele tukavipige, vinanda, ngoma, vinubi piga.


Maoni - Toa Maoni

Organist jimnez Apr 19, 2021
Inapendeza

Toa Maoni yako hapa