Ingia / Jisajili

Nimekukosea Mungu Wangu

Mtunzi: LUCHAGULA NGASSA
> Mfahamu Zaidi LUCHAGULA NGASSA
> Tazama Nyimbo nyingine za LUCHAGULA NGASSA

Makundi Nyimbo: Kwaresma | Mafundisho / Tafakari

Umepakiwa na: NGASSA LUCHAGULA

Umepakuliwa mara 2 | Umetazamwa mara 0

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Nimekukosea Ee Mungu wangu, nikitafakari maisha yangu, ninakuomba unihururumie×2

1. Dhambi zangu zilikutesa pale msalabani, hukuwa na kosa lolote pia majeraha uliyoyapata unihurumie ni upotovu wangu.

2. Nimelemewa na mizigo, ya dhambi zangu, zinanisononesha, nimekuwa mfungwa wa dhambi nioshe kwa damu yako.

3. Ninapotaka kutenda mazuri natenda mabaya, bila maongozi yako Bwana nitashindwa, nitapotea Mungu wangu niokoe.

4. Unisaidie niweze kuyavumilia mapungufu ya wenzangu, huku nikitambua ya kwamba hata mimi ninayo mapungufu, na unipe moyo wa kuomba radhi na kuwasamehe walionikosea.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa