Ingia / Jisajili

Sadaka Ya Moyo Wangu

Mtunzi: F.s. Matemele
> Tazama Nyimbo nyingine za F.s. Matemele

Makundi Nyimbo: Sadaka / Matoleo

Umepakiwa na: Fulgence Stanslaus

Umepakuliwa mara 0 | Umetazamwa mara 0

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Kiitikio: 

Pokea, Pokea Bwana Sadaka ya Moyo wangu, ninayokutolea leo kwa moyo mkunjufu x2. Ni sadaka ya shukrani sadaka ya upendo (nakuomba), uiunganishe na dhabihu ya Mwanao mpendwa, dhabihu ya mwanao mpendwa x2.

Maimbilizi:

1. Ninakuja mbele yako Baba mwenye huruma, nimebeba yote Bwana uliyonijalia, Mapendo, matumaini, furaha na amani, naviweka madhabahuni viwe mali yako. 
2. Pamoja na mkate huu na divai takatifu, napokea mwito Bwana wa kujitoa kwako, nitakase moyoni mwangu kwa Roho Mtakatifu, nifanye sadaka safi inayokupendeza.

3. Ninakushukuru Baba kwa wema wako mkuu, kwa vipaji vyote ulivyonijalia, vitumike (leo) na daima kuwahudumia wote, nakulitukuza ji-na lako mi-lele.

4. Ee Yesu wangu nifundishe kukupenda, nijitoe kwa ukarimu kama ulivyojitoa, Maisha yangu yawe sifa na ibada, mpaka siku nione utukufu wako Ee Bwana, hata niuone utukufu wako.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa