Maneno ya wimbo
KIT
B/T: Sauti ya mtu aliaye nyika ni inasema
All: (Itengenezeni njia (inasema) itengenezeni njia (inasema) itengenezeni njia ( bwana Yesu) apite (na yanyosheni) yanyosheni mapito yake (yanyosheni) yanyosheni mapito yake (yanyosheni)
yanyosheni mapito yake (bwana Yesu) aingie) X 2
MASHAIRI
1. S&A: Kila bonde litajazwa (na milima) na milima itashushwa (na palipo) Palipopotoka patanyoshwa, palipokwaruzwa patalainishwa.
2. B&T: Na wote walio na Mwili wataona wokovu watauona wokovu wake mwenye enzi
KILELE/HITIMISHO(CLIMAX)
G: Basi Yohana asema nini katika ujumbe wake wa toba?
L: Mwenye kanzu mbili ampe asiye nayo
G: Na watoza ushuru je?
L: Msitoze Zaidi ya mlivyoamriwa
G: Na askari je?
L: Msidhulumu wala kushtaki kwa uongo
ALL: Tuwe safi kumpokea (Bwana Yesu) Tutayarishe Nyoyo zetu (nyoyo zetu) bwana akija atupate sisi tutayari.
Nyimbo nyingine za mtunzi huyu