Ingia / Jisajili

Uturehemu Ee Bwana

Mtunzi: Aloyce Sagise
> Mfahamu Zaidi Aloyce Sagise
> Tazama Nyimbo nyingine za Aloyce Sagise

Makundi Nyimbo: Zaburi

Umepakiwa na: Aloyce Sagise

Umepakuliwa mara 7 | Umetazamwa mara 6

Wimbo huu unaweza kutumika:
- Katikati Dominika ya 1 ya Kwaresma Mwaka A

Download Nota
Maneno ya wimbo
Uturehemu Ee bwana. kwa kuwa tumetenda dhambi. 1.Ee Bwana unirehemu sawa sawa na fadhili zako kiasi cha wingi wa rehema zako uyafute makosa yangu unioshe kabisa na uovu wangu, unitakase dhambi yangu. 2.Maana nimejua mimi makosa yangu, na dhambi yangu I mbele yangu daima nimekutenda dhambi wewe peke yako, na kufanya MAOVU mbele ya macho yako. 3.Ee Mungu uniumbie moyo safi, uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu, usinitenge na uso wako wala roho wako Mtakatifu usiniondolee. 4.Unirudishie furaha ya wokovu wako unitegemeze kwa roho ya wepesi. Ee Bwana uifumbue midomo yangu na kinywa changu kitazinena sifa zako.

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa