Ingia / Jisajili

Ee_Bwana_Fadhili_Zako By C. Modest

Mtunzi: Thomas J.Yotham
> Mfahamu Zaidi Thomas J.Yotham
> Tazama Nyimbo nyingine za Thomas J.Yotham

Makundi Nyimbo: Zaburi

Umepakiwa na: Thomas Yotham

Umepakuliwa mara 0 | Umetazamwa mara 0

Wimbo huu unaweza kutumika:
- Katikati Dominika ya 21 Mwaka A

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo


Ee Bwana Fadhili zako ni za milele ((K): Zab. 137:8) Mtunzi: mwl Modest charles 


Kiitikio:

Ee Bwana, fadhili zako ni za milele; Usiziache kazi za mikono yako.

Mashairi. (Zaburi ya 137: 1-3, 6, 8b)

  1. Nitakushukuru kwa moyo wangu wote, mbele ya miungu nitakuimbia zaburi. Nitasujudu nikilikabili hekalu lako takatifu.
  2. Nitalishukuru jina lako, kwa ajili ya fadhili zako na uaminifu wako; kwa maana umeikuza ahadi yako kuliko jina lako lote. Siku ile niliyokuita uliniitikia, ukanifariji nafsi kwa kunitia nguvu.
  3. Ingawa bwana yuko juu, amwona mnyenyekevu, naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali. Ee Bwana fadhili zako ni za milele; usiziache kazi za mikono yako

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa