Ingia / Jisajili

MAISHA YANGU NI SALA

Mtunzi: Gerald Cuthbert
> Mfahamu Zaidi Gerald Cuthbert
> Tazama Nyimbo nyingine za Gerald Cuthbert

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari | Miito | Ndoa | Shukrani

Umepakiwa na: Gerald Cuthbert

Umepakuliwa mara 339 | Umetazamwa mara 1,163

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Mashairi:

1.  Nikikumbuka Maisha niliyopitia, Toka nizaliwe yananiumiza Mungu wangu,Ni maisha ya shida na tabu ndani yangu, leo moyo wangu waimba neema zake Mungu.

Chorus:

Ni Neema zake Mungu (na) ni Neema zake, Si mimi sio nguvu zangu ni Neema zake Mungu.Ni Neema zake Mungu (na) ni Neema zake, Si mimi sio nguvu zangu ni Neema zake!

2.   Ee Mungu wangu unihurumie mimi sasa, Wewe uliyeniumba mimi pasipo kujua,Unikomboe mimi nilipopotea, Ninapoanguka naamini wewe huniachi. 

3.   Na dunia hii sio yetu Bwana Mungu, Sasa nakuomba ziangazie hatua zanguNa roho yangu roho iliyopondeka, Uiepushie maovu ya humu duniani.


4.   Haya maisha bila yesu mimi ni bure, Nimejaribu tena ni mengi yameshindikana,We anza naye katika unalofanya,Maliza na yeye utaona Neema za Mungu.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa