Ingia / Jisajili

Sheria Yako Naipenda

Mtunzi: Nkana G.
> Tazama Nyimbo nyingine za Nkana G.

Makundi Nyimbo: Zaburi

Umepakiwa na: Goliath Nkana

Umepakuliwa mara 0 | Umetazamwa mara 0

Wimbo huu unaweza kutumika:
- Katikati Dominika ya 17 Mwaka A

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Kiitikio: Sheria yako naipenda mno ajabu X2

Sheria ya ko, sheria yako naipenda mno ajabu X2

1. Bwana ndiye aliye fungu langu, nimesema kwamba nitayatii maneno yako. Sheria ya kinywa chako ni njema kwangu, kuliko maelfu ya dhahabu na fedha.

2. Nakuomba, fadhili zako ziwe faraja kwangu sawasawa na ahadi yako kwa mtumishi wako. Rehema zako zinijie nipate kuishi, maana sheria yako ni furaha yangu.

3. Ndio maana nimeyapenda maagizo yako kuliko dhahabu, naam, dhahabu iliyo safi. Maana nayaona mausia yako yote kuwa ya adili, kila njia ya uongo naichukia.

4. Shuhuda zako ni za ajabu, ndio maana roho yangu imezishika. Kufafanusha maneno yako kwatia nuru, na kumfahamisha mjinga.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa