Mtunzi: Stephen Nguu
> Mfahamu Zaidi Stephen Nguu
> Tazama Nyimbo nyingine za Stephen Nguu
Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari | Tenzi za Kiswahili
Umepakiwa na: Stephen Nguu
Umepakuliwa mara 0 | Umetazamwa mara 0
Download Nota Download MidiTEMBEA NAMI
1.Ewe Mungu Bwana,Mungu mwenye Huruma,Naomba Uwe nami,katika maisha yangu,uwe mwamba na Nguvu,unilinde salama,nami nitakusifu siku zote za maisha yangu.
Mungu Baba Mwenyezi,ninakuomba Bwana,Simama nami Bwana siku zote zangu,tembea nami Bwana Mungu wewe ndiwe kinga yangu(ewe)x2
2. Kila niamkapo, matumaini yangu, ni kwako Bwana Mungu, ndiwe tumaini langu, kilaninachofanya, ninaomba neema, Mungu wangu simama nami niweze kufanikiwa.
3. Ikiwa nalemewa,uwe mwamba na Nguvu,uwe sitara yangu, katika safari yangu, katika mapito,uniongoze Bwana,niwe imara Bwana kwani ndiwe tumaini langu.
4. Harakatini zangu, katika kutafuta, Riziki yangu Bwana, unitangulie Bwana.Matatizo kazini, nipe hekima yako, nipe Na ujasiri kuifanya inavyonipasa. Hitimisho (Tembea nami Bwana, Tembea nami Mungu, wewe ndiwe tengemeo, ndiwe tumaini langu, Tembea nami Bwana daima Na milele) x2
Hitimisho
(Tembea nami Bwana, Tembea nami Mungu, wewe ndiwe tengemeo, ndiwe tumaini langu, Tembea nami Bwana daima Na milele) x2