Ingia / Jisajili

TUNAKUSHUKURU.

Mtunzi: Erick Wakusongwa
> Mfahamu Zaidi Erick Wakusongwa
> Tazama Nyimbo nyingine za Erick Wakusongwa

Makundi Nyimbo: Shukrani

Umepakiwa na: Erick Wakusongwa

Umepakuliwa mara 471 | Umetazamwa mara 1,251

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo
TUNAKUSHUKURU. Tunakushukuru Mpaji wa vyote, Ee Bwana Yesu asante, kwa mema yako uliyotujalia, twakuomba ukae nasi , (ulinde roho zetu x 2), na upokee shukrani zetu twaomba (na upokee shukrani zetu pokea x 2) Mashairi 1. Upendo wako kweli ni wa ajabu, umetulisha mwili wako na kutunywesha damu yako, Asante Ee Bwana Yesu kwa karamu uliyotujalia. 2. Upendo wako kweli ni wa ajabu, Ee Bwana Yesu umetujalia uzima wa mwili na roho, moyo wangu unajaa furaha siku zote. 3. Upendo wako kweli ni wa ajabu, ulisema aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu, hukaa ndani yangu nami hukaa ndani yake. 4. Upendo wako kweli ni wa ajabu, umetujalia neema ya Karamu ya chakula cha mbinguni wote tuliompokea, tumezipata neema zake.

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa