Mtunzi: Paschal Florian Mwarabu
> Tazama Nyimbo nyingine za Paschal Florian Mwarabu
Makundi Nyimbo: Juma Kuu
Umepakiwa na: respiqusi mutashambala
Umepakuliwa mara 0 | Umetazamwa mara 0
Download Nota Download MidiUmefanya kosa gani Yesu wangu; Umefanya kosa gani Bwana wangu; Kushitakiwa bure, kuteswa mpaka kufa msalabani umefanya kosa gani kweli ni huzuni sana Mungu wangu.
1. Kama dhambi mimi ndiye mwenye dhambi, kama kosa mimi ndiye mkosefu, wateseka kitu gani Bwana wangu.
2. Pilati hukumu gani ya uoga, asema haoni kosa kwako Bwana, lakini akuachia kuteseka.
3. A skari wafurahia hukumu, kwa dhihaka na dharau wakucheka, wakupiga uliye mwema milele.
4. M salaba mzito umeubeba, mijeledi bila huruma kupigwa, kisa gani mateso makali hayo.
5. Siyo Wewe Bwana siyo ila mimi, ndiye mwenye ku----stahili hukumu, kwa sababu mimi ndiye mwenye dhambi.
6. Umekubali mateso kwa uchungu, hata kufa kwaa huzuni msalabani, unihurumie Ewe Yesu wangu.