Ingia / Jisajili

Umefanya Kosa Gani Yesu Wangu

Mtunzi: Paschal Florian Mwarabu
> Tazama Nyimbo nyingine za Paschal Florian Mwarabu

Makundi Nyimbo: Juma Kuu

Umepakiwa na: respiqusi mutashambala

Umepakuliwa mara 0 | Umetazamwa mara 0

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Umefanya kosa gani Yesu wangu; Umefanya kosa gani Bwana wangu; Kushitakiwa bure, kuteswa mpaka kufa msalabani umefanya kosa gani kweli ni huzuni sana Mungu wangu.

1. Kama dhambi mimi ndiye mwenye dhambi, kama kosa mimi ndiye mkosefu, wateseka kitu gani Bwana wangu.

2. Pilati hukumu gani ya uoga, asema haoni kosa kwako Bwana, lakini akuachia kuteseka.

3. A   skari wafurahia hukumu, kwa dhihaka na dharau wakucheka, wakupiga uliye mwema milele.

4. M salaba mzito umeubeba, mijeledi bila huruma kupigwa, kisa gani mateso makali hayo.

5. Siyo Wewe Bwana siyo ila mimi, ndiye mwenye ku----stahili hukumu, kwa sababu mimi ndiye  mwenye dhambi.

6. Umekubali mateso kwa uchungu, hata kufa kwaa huzuni msalabani, unihurumie Ewe Yesu wangu.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa