Ingia / Jisajili

Acheni Kukata Tamaa

Mtunzi: Bernard Mukasa
> Mfahamu Zaidi Bernard Mukasa
> Tazama Nyimbo nyingine za Bernard Mukasa

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari

Umepakiwa na: Yudathadei Chitopela

Umepakuliwa mara 13,039 | Umetazamwa mara 27,354

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Mwenyezi ameniumba akanileta kati yenu niwakumbushe watu wake thamani yenu duniani x2

Acheni kufa moyo acheni kukata tama yeye aliyewaumba anaijua kazi yakex2

1.       Aliijua siri yenu hata kabla hamjaumbwa ramani ya maisha yenu yote imo mikononi mwake

2.       Magonjwa yanayo watesa na maumivu yasiyo koani madogo kuliko yale aliyoyaponya kwa sekunde

3.       Hali mbaya ya kiuchumi mlo mmoja madeni mengi ni njia ya kunyenyekeana kumpa Mungu utukufu

4.       Misiba inayowaliza mnapofiwa na ndugu zenu ni njia ya wapendwa wenu kwenda mbinguni wakafurahi

5.       Maumivu yakuonewa kudhulumiwa kusingiziwa ni njia ya wapendwa wenu kwenda mbinguni wakafurahi

6.       Matatizo ya ndoa zenu na migogoro ya familia ni bahati mmejaliwa ya kujifunza uvumilivu

7.       Nadhili ngumu za utawa, misukosuko ya ukasisi ni kuuvua ulimwengu na kulivaa koti la uwingu

8.       Bebeni misalaba yenu nyamazeni msinung’unike huo ndio wokovu wenu shikilieni msiachie


Maoni - Toa Maoni

francis Dec 03, 2019
Upo sawa kabisa. beti la 5 na la 8 ziko na kasoro kwenye mpangilio. zirekebishwe ziendanishe na maneno kwenye pdf

FRANK C L Feb 15, 2019
BETI LA NNE NA LA TANO NAHISI MANENO HAYO YANA SHIDA KIDOGO

Michael Deusdedit Kidutu Aug 16, 2018
Nimeipenda hiyo, na mm kutoka familia ya kimaskini so imenipa moyo wa kusongambele zaid ktk kila jambo, make kila litendekalo ni yeye ndiye kalipanga.

Michael kidutu Aug 16, 2018
Hongera sana, kiukwel uko vizur ongeza juhud iwe zaid ya hapo.

James Benjamin May 01, 2018
Hongera Sana, ubarikiwe

Yohana Moses Oct 03, 2017
Hongera Bro, natamani nana na mimi niujue mziki siku moja...

Deodath Nombo Oct 01, 2017
Uko vizuri sana na kitengo chako Mungu aendelee kukupa hekima na zaidi ili Mungu atukuzwe zaidi

NGWESA Jun 30, 2017
kaka kristu unafanya kazi vyema endelea hivohivo ila nahitaji na mimi unisaidi kujua mziki nipo jimbo kuu la mwanza parokia ya buzuruga 0754237836

Joseph Were Oct 17, 2016
Ninazipenda hizi nyimbo na kweli ni nazitumia kanisani kwenye sala na kuabudu.

Isdory Sep 19, 2016
Hongela Kaka Kwa Utnzi Wa Nyimbo

Gaston Tubunda Sep 07, 2016
Uwe mstaarabu

May 15, 2016
Kweli Kwa Utunzi Wako Nyimbo Za Rc Mungu Amekujalia

May 03, 2016
Tunashukuru sana kwa kuweza kufikia kiwango cha utandawazi. Kwa kuwa mimi kama mrundi kuupata wimbo huu ingekuwa vigumu sana. Mpaka nipande boat au ndege. Ila kwa sasa mambo yamekuwa rahisi sana. Tunamuomba mungu hata na sisi atuwezeshe kufikia angalau level ambayo hata na ninyi mnaweza kuzipata za kwetu pia. Hongera sana admin na wale mnao upload mungu awajalie neema na baraka tele muwe na mafanikio mema.

Toa Maoni yako hapa