Ingia / Jisajili

Bwana ni tegemeo langu

Mtunzi: Dr. Charles N. Kasuka
> Mfahamu Zaidi Dr. Charles N. Kasuka
> Tazama Nyimbo nyingine za Dr. Charles N. Kasuka

Makundi Nyimbo: Zaburi

Umepakiwa na: Mika Wihuba

Umepakuliwa mara 195 | Umetazamwa mara 1,069

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Bwana alikuwa tegemeo langu, tegemeo langu, akanitoa akanipeleka panapo nafasi x2 Akaniponya, kwa kuwa Bwana, alikuwa kapendezwa nami, Alikuwa amependezwa nami x2.

1.Bwana alinitendea Sawasawa na Haki yangu, Sawasawa na Usafi wa Mikono yangu. Kwa maana nimezishika Njia za Bwana, Wala sikumuasi Mungu wangu.

2.Hukumu zake zote zilikuwa ziko mbele yangu, Wala Amri zake sikujiepusha epusha nazo. Nami nilikuwa mkamilifu mbele zake, nikajilinda na uovu wangu.

3.Kwa mtu mwenye Fadhili utakuwa mwenye Fadhili, kwa mkamilifu utajionyesha ukamilifu. Kwake ajitakaye, utajionyesha, na kwa mpotevu kuwa mkaidi.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa