Ingia / Jisajili

Dhabihu Ya Moyo Wangu

Mtunzi: Emily Mushi
> Mfahamu Zaidi Emily Mushi
> Tazama Nyimbo nyingine za Emily Mushi

Makundi Nyimbo: Shukrani

Umepakiwa na: Emily Mushi

Umepakuliwa mara 0 | Umetazamwa mara 0

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

KIITIKIO:Ninakushuru Mungu Baba Mwenyezi kwa zawadi ya Maisha ulonipa mtumishi wako, Ninakushukuru na kwa karama zangu zote ulizonipa Mungu wangu kwa ajili ya kazi zako.Dhabihu ya moyo wangu, nikushukuru Mungu wangu, sina kitu chakulipa kufidia Fadhili zako,Nakuomba Baba, uzidi kunisimamia nitimize upendo wako kufadhili wenye shida.


MABETI
1. Katika kuishi kwangu nimepata maumivu, nikakata na tamaa, magonjwa kuniandama,lakini Ewe Mungu wangu ukanirehemu, ukanifunza moyo kuwa wewe ni Mungu wa kweli.

2. Damu takatifu yake Yesu ni Uzima, tunapaswa kuishi kwa kutumaini Damu yake (Bwana)Yesu, hii ni uthaminisho tuliopewa na Mwenyezi Mungu.

3. Sitakufa bali nitaishi nikiyasimulia, nikiyasimulia matendo yako Bwana Mungu wangu, nakuutangaza ukuu wako kwa mataifa, wakutukuze wewe wakiamini wewe ndiwe Mungu.




Nyimbo nyingine za mtunzi huyu

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa