Mtunzi: Emily Mushi
> Mfahamu Zaidi Emily Mushi
> Tazama Nyimbo nyingine za Emily Mushi
Makundi Nyimbo: Pasaka
Umepakiwa na: Emily Mushi
Umepakuliwa mara 2 | Umetazamwa mara 0
Download Nota Download MidiKiitikio:
Tuelezee Mariamu uliona nini kaburini (ORGAN) Nilikuta jiwe limeviringishwa pembeni, nilimkuta Malaika wa Mungu akaniambia: Yesu Mnazareti aliyesulubiwa amefufuka; (njoni mpatazame alipokuwa amelazwa, Amefufuka Aleluya Aleluya)x2
Mabeti:
1 (a). Nendeni upesi mkawambie wanafunzi; Amefufuka Aleluya Aleluya,
(b). Awatangulia kwenda zake Galilaya; Amefufuka Aleluya Aleluya.
2 (a). Wakakaribia wakamsujudia; Amefufuka Aleluya Aleluya,
(b)Msiogope kawambieni ndugu zangu; Amefufuka Aleluya Aleluya.
3 (a). Amepewa mamlaka duniani na Mbinguni; Amefufuka Aleluya Aleluya,
(b) Mkabatize kwa maji na Roho Mtakatifu; Amefufuka Aleluya Aleluya.
4. Amefufuka Bwana Yesu ni mzima, kashinda mauti kaleta uzima, (kaushinda uovu wote twimbe Aleluya)x2