Ingia / Jisajili

Tuelezee Maria

Mtunzi: Emily Mushi
> Mfahamu Zaidi Emily Mushi
> Tazama Nyimbo nyingine za Emily Mushi

Makundi Nyimbo: Pasaka

Umepakiwa na: Emily Mushi

Umepakuliwa mara 2 | Umetazamwa mara 0

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Kiitikio:

Tuelezee Mariamu uliona nini kaburini (ORGAN) Nilikuta jiwe limeviringishwa pembeni, nilimkuta Malaika wa Mungu akaniambia: Yesu Mnazareti aliyesulubiwa amefufuka; (njoni mpatazame alipokuwa amelazwa, Amefufuka Aleluya Aleluya)x2

Mabeti:

1 (a). Nendeni  upesi mkawambie wanafunzi; Amefufuka Aleluya Aleluya,

  (b). Awatangulia kwenda zake Galilaya; Amefufuka Aleluya Aleluya.

2 (a). Wakakaribia wakamsujudia; Amefufuka Aleluya Aleluya,

   (b)Msiogope kawambieni ndugu zangu; Amefufuka Aleluya Aleluya.

3 (a). Amepewa mamlaka duniani na Mbinguni; Amefufuka Aleluya Aleluya,

   (b) Mkabatize kwa maji na Roho Mtakatifu; Amefufuka Aleluya Aleluya.

4. Amefufuka Bwana Yesu ni mzima, kashinda mauti kaleta uzima, (kaushinda uovu wote twimbe Aleluya)x2


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa