Mtunzi: Eng.Richard Samson
> Mfahamu Zaidi Eng.Richard Samson
> Tazama Nyimbo nyingine za Eng.Richard Samson
Makundi Nyimbo: Zaburi
Umepakiwa na: Richard Samson
Umepakuliwa mara 1 | Umetazamwa mara 0
Wimbo huu unaweza kutumika:
- Katikati Dominika ya 31 Mwaka C
Ee Mungu Mfalme wangu,
Nitalitukuza jina lako milele x2
(AU)
Ee Mungu Wangu Mfalme Nitakutukuza,
Nitalihimidi Jina Lako Milele x2.
1. Ee Mungu wangu, Mfalme, nitakutukuza,
Nitalihimidi jina lako milele na milele.
Kila siku nitakuhimidi,
Nitalisifu jina lako milele na milele.
2. Bwana ana fadhili, ni mwingi wa huruma,
Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema,
Bwana ni mwema kwa watu wote,
Na rehema zake zi juu ya viumbe vyake vyote.
3. Ee Bwana, viumbe vyako vyote vitakushukuru,
Na wacha Mungu wako watakuhimidi.
Wataunena utukufu wa ufalme wako.
Na kuuhadithia uweza wako.
4. Ufalme wako ni ufalme wa zamani zote,
Na mamlaka yako ni ya vizazi vyote.
Bwana huwategemeza wote waangukao,
Huwainua wote walioinamia chini.