Ingia / Jisajili

Moyo Mt. Wa Yesu Somo Wa Kwaya Yetu

Mtunzi: Benny Weisiko John
> Mfahamu Zaidi Benny Weisiko John
> Tazama Nyimbo nyingine za Benny Weisiko John

Makundi Nyimbo: Moyo Mtakatifu wa Yesu

Umepakiwa na: Benny Weisiko

Umepakuliwa mara 794 | Umetazamwa mara 3,237

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

KIITIKIO

Moyo Mtakatifu wa Yesu Kristo (Ewe) uliye msimamizi (na somo) wa kwaya yetu, utuhurumie sisi wanao.

Moyo Mtakatifu wa Yesu Kristo (Ewe) uliye msimamizi (na somo) wa kwaya yetu, utupiganie sisi wanao.

[Tunapokusanyika (kwa pamoja) mahali popote (Yesu),

Tunapokusanyika (kwa pamoja) uwe kati yetu (daima) utukinge kwa Damu yako dhidi ya shetani mwovu.]x2

SHAIRI (ALTO &SUPRANO)

1.Kwa Damu yako Takatifu Ee Yesu, utupe nguvu tushinde vishawishi, tukutumikie wewe kwa sauti        za kuimba, (daima) tutangaze neno lako kwa kuimba.

2. Utujalie tudumishe upendo, tuwasamehe wanaotukosea, utujalie baraka katika maisha yetu, (nasi) tutembee kwa furaha ndani yako

SHAIRI (TENO & BASS)

3. Sauti zetu hizi zinazovuma kwa kishindo, ziambatane na nguvu zako kutoka Mbiguni,

  ziwashe moto hapa katikati yetu, zifukuze giza pia na pepo wachafu, Njoo Yesu kaa nasi.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa