Ingia / Jisajili

Msaada Wangu U Katika Bwana

Mtunzi: Eng.Richard Samson
> Mfahamu Zaidi Eng.Richard Samson
> Tazama Nyimbo nyingine za Eng.Richard Samson

Makundi Nyimbo: Zaburi

Umepakiwa na: Richard Samson

Umepakuliwa mara 0 | Umetazamwa mara 0

Wimbo huu unaweza kutumika:
- Katikati Dominika ya 29 Mwaka C

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Msaada wangu u katika Bwana, Aliyezifanya mbingu na nchi X2.

1. Nitayainua macho yangu niitazame milima;
Msaada wangu utatoka wapi?
Msaada wangu u katika Bwana,
Aliyezifanya mbingu na nchi.

2. Asiuache mguu wako usongezwe,
Yeye akulindaye asisinzie.
Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi,
Yeye aliye mlinzi wa Israeli.

3. Bwana ndiye mlinzi wako;
Bwana ni uvuli, husimama mkono wako wa kuume,
Jua halitakupiga mchana,
Wala mwezi wakati wa usiku.

4. Bwana atakulinda na mabaya yote,
Atakulinda nafsi yako.
Bwana atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele. 


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa