Ingia / Jisajili

Nitakutukuza Mungu

Mtunzi: S. E. Mlugu
> Tazama Nyimbo nyingine za S. E. Mlugu

Makundi Nyimbo: Shukrani

Umepakiwa na: Martin Munywoki

Umepakuliwa mara 2,693 | Umetazamwa mara 5,044

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Kwa kinywa changu Mungu wangu nitakutukuza,

kwa nyimbo nzuri nitaziimba sifa (zako )

Kwa kuwa Mungu wema wako kwangu mimi ni mkuu siwezi kuelezea

{ Sina kitu Bwana cha kukupa (wewe)

kulingana na mema uloyatenda

Naitoa kwako nafsi yangu (Bwana)

nitendee unavyotaka } *2


1. Kama ni pumzi ya uhai umenipa bure,

Sauti nzuri ya kuimbia, yatoka kwako

Nakurudishia sifa na shukrani


2. Kama ni elimu, niliyo nayo ni mali yako,

Ujuzi na kazi niliyo nayo vyatoka kwako

Nakurudishia sifa na shukrani


3. Magonjwa mengi umeniponya ee Mungu wangu,

Na ajali nyingi umenikinga ee Mungu wangu

Nakurudishia sifa na shukrani


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa