Ingia / Jisajili

Nitamhimidi Bwana Kila Wakati

Mtunzi: Melchior Basil Syote
> Tazama Nyimbo nyingine za Melchior Basil Syote

Makundi Nyimbo: Zaburi

Umepakiwa na: lucas mlingi

Umepakuliwa mara 3,144 | Umetazamwa mara 8,327

Download Nota
Maneno ya wimbo

NITAMHIMIDI BWANA KILA WAKATI

Nitamhimidi Bwana kila wakati, sifa zake zi kinywani mwangu daima katika Bwana nafsi yangu itajisifu wanyenyekevu wasikie wakifurahi (mtukuzeni Bwana) mtukuzeni Bwana pamoja nami na tuliadhimishe jina lake pamoja. (Malaika wa Bwana hufanya kituo) akiwazungukia wamchao nakuwaokoa., onjeni mwone yakuwa Bwana yu mwema heri mtu yule anayemtumaini. (Mcheni Bwana)enyi Watakatifu wake yaani wamchao hawahitaji kitu. Njooni enyi waana mnisikilize (njooni) nami nitawafundisha kumcha Bwana uzuie ulimi wako na mabaya na midomo yako na midomo yako na kusema hila uache mabaya utende mema Bwana huzikumbuka nafsi za watumishi wake wala hawatahukumiwa wote wanaomkimbilia Bwana.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa