Mtunzi: Justine Mgobela
> Mfahamu Zaidi Justine Mgobela
> Tazama Nyimbo nyingine za Justine Mgobela
Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari | Ndoa
Umepakiwa na: Justine Mgobela
Umepakuliwa mara 8 | Umetazamwa mara 16
Download Nota Download MidiTutambue "UMUHIMU WA SAKRAMENTI YA NDOA" ili tuishi katika familia zetu kwa pendo la Mungu;
Mt.Paulo anatuhimiza sakramenti ya ndoa hutuletea Baraka takatifu ya Mungu asili ya pendo lake;
Wakristo tuache uchumba sugu kwa maana mume asiyeamini hutakaswa katika mke wake, kwa maana mke asiye amini hutakaswa katika mume wake;
Kila mwanaume awe na mke wake mwenyewe na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe, shetani asije kutujaribu kwa kutokuwa na nafasi kwetu;
Familia takatifu ni familia yenye Baraka, hiyo ndiyo familia bora yenye misingi ya kikristo, Hiyo hudumu katika, katika pendo la Mungu, watoto ndani ya nyumba huwa na malezi bora;
"UMUHIMU WA SAKRAMENTI YA NDOA"
1.Iwe chachu ya upendo,
2.Iwe chachu ya furaha,
3.Iwe chachu ya Amani;
Na ahimidiwe Baba wa Bwana wetu Yesu kristo, Baba wa rehema, Mungu wa faraja yote kwa maana ndiye atufanyaye kuwa imara;
Tumwamini kristo awe ndani yetu tupate kudumu ndani ya pendo lake;
Wakristo wote tunapaswa kutambua kwamba, Ndoa ni ya mke mmoja (pia) ndoa ni ya mume mmoja.