Ingia / Jisajili

Mungu Asiyeshindwa

Mtunzi: Stephen Nguu
> Mfahamu Zaidi Stephen Nguu

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari

Umepakiwa na: Stephen Nguu

Umepakuliwa mara 7 | Umetazamwa mara 12

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

MUNGU ASIYESHINDWA

Utangulizi:

Ni wewe Mungu Muumba wangu ni wewe Bwana Ngome yangu ni wewe Bwana,wewe Bwana Mungu,(Tena)Ni wewe mwenye kuutawala Mbinguni hata Duniani ni wewe Bwana,wewe Bwana Mungu,(kweli)Ni wewe mwenye Mamlaka usiyeshindwa na chochote ni wewe Bwana,wewe Bwana Mungu,wewe Mungu Mkuu.

chorus:Ni wewe Bwana Mungu(wangu),uliyenishindia (wewe)ukanipigania mimi nikawa mjasiri,ukanipa uweza(mimi)nikasimama tena (wewe)ukawa nguvu yangu Mungu nakushukuru sana,{(Mungu)wewe ni wa upendo(kweli)nikupe nini Bwana (Mungu)zaidi ya upendo(kwani)Maisha yangu mimi(tena)kuishi kwangu mimi(Mungu)ni kwa upendo wako}x2

Mashairi:

1.Kwa maana kwangu mimi,kuishi ni Kristo nao,kufa kwangu ni faida,kama nitaendelea,kuishi katika mwili,hii itaniwezesha kufanya kazi yenye matunda.

2.Nakabiliwa na haya, mawili yasiyo sawa,natamani kuyaacha,maisha haya niende, nikakae naye Kristo,pamoja naye Kristo,Bora zaidi,siku zote.

3.Wanaoamini Kristo,fanyeni kazi ya Kristo,wahubirieni watu,ili wote wamjue,hiyo ndiyo kazi kuu, aliyotuachia,wajulisheni,wafundisheni.

Hitimisho:

Ni wewe uliyewavusha wana wa israeli(kwenye)Bahari ya shamu wakavuka kwenye nchi kavu,

Ni wewe uliyewashushia mana toka Mbingu(tena)ukawalisha nafaka ya Mbinguni E Bwana Mungu

(Wewe ni Mungu mkuu,usiyeshindwa na ni wewe mwenye uwezo Enzi Utukufu pokea Sifa,Wewe ni ALFA OMEGA, mwanzo na Mwisho Usifiwe Mungu Mwenyezi siku zote hata Milele)x2


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa