Ingia / Jisajili

Ninakuabudu Mungu Wangu (Adoro Te) Acc. Dbw

Mtunzi: Traditional
> Tazama Nyimbo nyingine za Traditional

Makundi Nyimbo: Juma Kuu

Umepakiwa na: David Wasonga

Umepakuliwa mara 3,088 | Umetazamwa mara 8,092

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

1.Nakuakuabudu Mungu wangu ujifichaye altareni,ninakutolea moyo wangu usiofahamu siri yako (Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu milele, milele milele u mtakatifu, utukuzwe milele yote katika Hostia Takatifu

2.Mafahamu yangu yadanganya yakwunapo pia kugusa, nami ninakupa moyo wangu usiofahamu siri yako (Mtakatifu..........)

3.Wauficha u-Mungu wako msalabani na ubinadamu wako altareni, nami naungama yote mbili kama mwivi yule mwenye toba (Mtakatifu.....)

4.Thomaso aligusa majeraha nami nasadiki bila shaka,Ee Yesu nipe pendo lako nikwamini wewe kwa imani. (Mtakatifu......)

5.Umeteswa nini bwana mwema kwa kunipa mkate wa uzima, Yesu unifiche ndani yako ili nionje pendo lako(Mtakatifu.....)

6.Yesu pelicane utazame na kwa damu yako nitakase, tone moja ndilo lanitosha na dunia yote yaokoka (Mtakatifu....)

7.Ndani ya mafumbo Yesu yumo utafunguliwa kwangu lini,nikuone Yesu uso wako nishiriki nawe heri yako (Mtakatifu.....)


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa