Ingia / Jisajili

Sadaka Twakutolea Leo Ni Zawadi

Mtunzi: Alphonce Andrew Otieno Obonyo
> Mfahamu Zaidi Alphonce Andrew Otieno Obonyo
> Tazama Nyimbo nyingine za Alphonce Andrew Otieno Obonyo

Makundi Nyimbo: Sadaka / Matoleo

Umepakiwa na: Alphonce Andrew Otieno Obonyo

Umepakuliwa mara 0 | Umetazamwa mara 0

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

SADAKA TWAKUTOLEA LEO NI ZAWADI

Ee Bwana, upokee sadaka yetu,
Tunayoileta mbele zako leo.
Sadaka twakutolea leo ni zawadi,
Toka mikononi mwako twakuomba
(Upokee upokee upokee, kwa upendo)2.

1.Abeli alimtokea Bwana,
Malimbuko ya kondoo sadaka yake kwa upendo.
Nasi twaleta yaliyo mema mbele ya Bwana,
Pokea sadaka yetu kama ya Abeli.

2.Ibrahimu alimwamini akatoa mwana wa pekee,
Mungu akafurahi naye
kwa imani yake Bwana alimbariki sana,
Nasi twaleta sadaka yetu kwa imani.

3.Mjane alimtolea vyote alivyo navyo 
Baraka ya Mungu alituzwa,
kwa moyo wake wote alimtolea mumbaye,
Sadaka tumtolee Bwana Mungu kwa upendo.

4.Melkizedeki alitoa mkate hata na divai,
Akambariki Ibrahimu.
Ibrahimu akatoa sehemu ya maliyo,
Nasi twaleta sadaka yetu kwako Bwana.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa