Ingia / Jisajili

Ee Mungu wangu Mfalme

Mtunzi: Emil E Muganyizi
> Tazama Nyimbo nyingine za Emil E Muganyizi

Makundi Nyimbo: Zaburi

Umepakiwa na: Emil Mwemezi

Umepakuliwa mara 1,606 | Umetazamwa mara 3,888

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Ee Mungu wangu Mfalme (Mfalme) nitakutukuza nitalihimidi jina lako milele na milele X2

01. Bwana ana fadhili ni mwingi wa huruma, si mwepesi wa hasira ni mwingi wa rehema, Bwana ni mwema kwa watu wote na rehema zake zi juu ya kazi zake zote.

02. Bwana kazi zako zote zitakushukuru, na wacha Mungu wako watakuhimidi, wataunena utukufu wa Ufalme wako na kuuhadithia uweza wako.

03. Ili kuwajulisha matendo yake makuu, na utukufu wa fahari ya ufalme wake, Ufalme wako ni ufalme wa zamani zote, na mamlaka yako ni ya vizazi vyote.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa