Ingia / Jisajili

Nimekuja Kuyafanya Mapenzi Yako (Ndipo Niliposema)

Mtunzi: Eng.Richard Samson
> Mfahamu Zaidi Eng.Richard Samson
> Tazama Nyimbo nyingine za Eng.Richard Samson

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari | Miito | Zaburi

Umepakiwa na: Richard Samson

Umepakuliwa mara 2 | Umetazamwa mara 0

Wimbo huu unaweza kutumika:
- Katikati Dominika ya 2 Mwaka A
- Katikati Dominika ya 2 Mwaka B

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Ndipo niliposema, Tazama nimekuja, tazama nimekuja kuyafanya mapenzi yako x2.

1. Nalimngoja Bwana kwa saburi,
Akaniinamia akakisikia kilio changu.
Akatia wimbo mpya kinywani mwangu
Ndio sifa zake Mungu wetu.

2. Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo,
Masikio yangu umeyazibua,
Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka.
Ndipo niliposema, Tazama nimekuja. 

3. Katika gombo la chuo nimeandikiwa,
Kuyafanya mapenzi yako,
Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu;
Naam, sheria yako imo moyoni mwangu. 

4. Nimehubiri habari za haki
Katika kusanyiko kubwa,
Sikuizuia midomo yangu;
Ee Bwana, unajua. 


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa