Ingia / Jisajili

Upendo Wa Kweli

Mtunzi: Fred B. Kituyi
> Tazama Nyimbo nyingine za Fred B. Kituyi

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari

Umepakiwa na: FRED KITUYI

Umepakuliwa mara 1,601 | Umetazamwa mara 4,680

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Kiitikio:

Bwana unifanye chombo cha amani,

nikaeneze kote kote ulimwenguni, tukaishi kwa amani. x2

(Palipo chuki nilete pendo, penye ugomvi nilete patano, (Ee!)               

Tupendane, tupendane kama vile Yesu anavyotupenda. x2)

1. Nikiwa nao upendo, nitaeneza amani:
(Sote tutaishi nayo furaha – furaha yake Mungu. x2)

2.  Upendo hauna chuki, upendo hauna wivu:
(Upendo wa kweli hutoka kwake - Mwenyezi Mungu Baba. x2)

3.  Upendo huvumilia, na hauoni mabaya:
(Ee Baba naomba nipe upendo - nipe nayo amani. x2)

4.  Nikiwa nayo imani, ya kuhamisha milima:
(Nisipokuwa na ule upendo - mimi ni kitu bure. x2)


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa