Ingia / Jisajili

HUYU NI MAMA MTAKATIFU VERONIKA

Mtunzi: Pascal Mussa Mwenyipanzi
> Mfahamu Zaidi Pascal Mussa Mwenyipanzi
> Tazama Nyimbo nyingine za Pascal Mussa Mwenyipanzi

Makundi Nyimbo: Tenzi za Kiswahili | Watakatifu

Umepakiwa na: Pascal Mussa

Umepakuliwa mara 263 | Umetazamwa mara 1,584

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo
HUYU NI MAMA Kiitikio: Huyu ni mama na somo wa kwaya yetu(huyu) huyu ni mama Mtakatifu veronika Msimamizi na mwombezi wa kanisa letu,Mama salamu mama mwema(mama) salamu veronika(mama)twakushangilia wewe ni mlinzi wetu(twaomba)utuombee tufike huko mbinguni. 1.Mama ulimpa Kristo kitambaa alichokitumia kupanguzia damu kutoka kwa uso wake,kwa ukarimu huo mkuu aliuacha wajihi wake Mtakatifu kwenye kitambaa hicho, tuombee Mama kwa Bwana wetu Yesu Kristo, wajihi wake uwe mioyoni mwetu. 2.Veronika Mtakatifu wewe ni somo wetu hakika, umekuwa kimbilio, msaada mama yetu, umekuwa msaada wetu veronika, wanakwaya tunajivunia ujasiri wako Mama; tunakuomba utupatanishe naye Mungu, ili familia zetu zifike mbinguni.

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa