Ingia / Jisajili

Kama Watoto Wachanga No.2

Mtunzi: Alex Rwelamira
> Mfahamu Zaidi Alex Rwelamira
> Tazama Nyimbo nyingine za Alex Rwelamira

Makundi Nyimbo: Mwanzo | Pasaka | Ubatizo

Umepakiwa na: Alex Rwelamira

Umepakuliwa mara 1,304 | Umetazamwa mara 3,696

Wimbo huu unaweza kutumika:
- Mwanzo Dominika ya 2 ya Pasaka Mwaka A
- Mwanzo Dominika ya 2 ya Pasaka Mwaka B
- Mwanzo Dominika ya 2 ya Pasaka Mwaka C

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa (Yatamanini maziwa, yatamanini maziwa, maziwa ya akili yasiyoghoshiwa (ili) ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu Aleluya)X2

  1. Pokeeni furaha ya utukufu wenu mshukuruni Mungu aliyewaita kwa ufalme wake wa mbinguni.
  2. Ahimidiwe Mungu Baba wa Bwana Yesu Kristo ambaye kwa rehema zake  alituzaa mara ya pili ili tupate tumaini lenye uzima kwa kufufuka kwake Yesu Kristo.
  3. Tupate na urithi usioharibika, usio na uchafu usionyauka uliotunzwa mbinguni.

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa