Maneno ya wimbo
                NIKUFANYE RAFIKI
1.	Kuna mambo mi' natakanikujuze yapo mengi ninahisi nikuambie 
kuhusu yaliyomo maishani mwangu, nisimulie maana wategasikio,
kama rafiki rafiki mwaminifu 
Wewe wanijua, unanifahamu, unanielewa, umenichunguza, 
Wanisikiliza, unanishauri, unanisamehe, wewe ni rafiki 
hivyo naomba nikufanye, rafiki yangu mwema, rafiki mwaminifu 
wewe uliyekamilika, nikamilishe mimi, kwa pendo lako wewe
2.	Nimekumbwa nayo masaibu tele, kajipata naegemeaya dunia,
nayo kanipotosha kaniangamiza, yakanifumba macho sikuoni tena 
lakini wewe ukanihurumia 
3.	Nilidhani raha ndiyo kila kitu, mle ndani niliona kwamba 'kafika,
sheria yako nayo sikuifuata, na pia yote yale ulonifundisha,
na bado utayari kunisamehe 
4.	Nikaona yote kawaida kwangu, afya njema lishe bora pia furaha,
ni kwa neema zako nimefanikiwa, kuishi vema pia kuyaona mema,
na hayo yote niwe wanijalia
            
                                    
                Nyimbo nyingine za mtunzi huyu